Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa zamani alaani mali zake kutwaliwa na utawala mpya
Kimataifa

Rais wa zamani alaani mali zake kutwaliwa na utawala mpya

Rais wa zamani wa Zambia, Edgar Lungu
Spread the love

WAKILI wa Rais wa zamani wa Zambia Edgar Lungu, amelaani hatua ya serikali ya nchi hiyo, kutwaa mali mbalimbali zinazohusishwa na familia mwanasiasa huyo, na kusema kuwa kitendo hicho kimechochewa kisiasa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Rais wa sasa wa Zambia Hakainde Hichilema amekuwa akikabiliana na ufisadi, lakini wakosoaji wanasema analenga wapinzani wake wa kisiasa.

Serikali ilitwaa rasmi mali hizo kutoka kwa familia ya Lungu wiki iliyopita, ambazo ni pamoja majengo 15 ya ghorofa mbili kila moja, nyumba ya kulala wageni ya gorofa tatu, shamba na nyumba ya kawaida. Mali hizo zilichukuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Utaifishaji wa Mapato ya Uhalifu ya mwaka 2010, ambayo inaruhusu serikali kutwaa mali ambayo inaamini ilipatikana kwa njia zisizo halali.

Wakili wa Rais huyo wa zamani, Makebi Zulu, aliiambia Sauti ya Amerika kwamba yeye wala wateja wake hawajapewa notisi ya mchakato wowote, ulio mbele ya mahakama yoyote kuhusu kukamatwa kwa mali hiyo.

Akizungumza na vyombo vya sheria tangu uchunguzi huo uanze mwaka jana, Zulu alisema wateja wake wametoa maelezo ya kutosha jinsi walivyopata mali hizo.

Alisema serikali inazuia kwa makusudi taarifa hizo ili kuwaaibisha Lungu, mke wake Esther Lungu, na watoto wao.

Wakosoaji wa Rais wanasema tangu serikali yake ilipoanza kuwakamata viongozi wa utawala uliopita na kuwafanyia uchunguzi wa madai ya vitendo vya rushwa, hakuna yeyote kati yao aliyepatikana na hatia yoyote.

Hichilema anasisitiza kuwa vita dhidi ya ufisadi havina maana ya kuwadhulumu wapinzani wake wa kisiasa.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!