Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkutano wa uhisani Afrika kuunguruma Zanzibar
Habari Mchanganyiko

Mkutano wa uhisani Afrika kuunguruma Zanzibar

Spread the love

MKUTANO wa nane wa uhisani Afrika Mashariki (EAPC), unatarajiwa kuanza kufanyika  tarehe 28  hadi 30 Juni 2023, visiwani Zanzibar.Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 27 Juni 2023 na Afisa Mtendaji Mkuu wa EAPC, Evans Okinyi, bodi za udhamini zinazofanya hisani, taasisi na mashirika yanayofanya kazi za kijamii pamoja na yanayotoa ruzuku kwa ajili ya miradi ya maendeleo Tanzania na nchi za Afrika Mashariki, zitashiriki mkutano huo.

“Mkutano huu ni kwa ajili ya kuhamasisha suala la uhisani katika jamii na kujadili namna bora kuendeleza uhisani barani Afrika, kwa ajili ya kuleta maendeleo. Mkutano huo unaendeshwa na Mtandao wa Uhisani Afrika Mashariki (East Africa Philanthropy Network – EAPN),  kwa kushirikiana na Legal Services Facility (LSF),” imesema taarifa ya Okinyi.

Mkutano huo unatarajiwa kuwa na washiriki 300, ambao watabadilishana uzoefu, kufanya tathimini ya pamoja na kuunda mipango ya kihisani na kijamii ili kuwekeza katika jamii barani Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!