WIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka wa fedha wa 2024/25 kiasi cha Sh. 2.72 trilioni, ikiwa ni ongezeko kutoka bajeti ya Sh. 2.08 trilioni iliyopitishwa 2023/24. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti hiyo, Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema Sh. 2.61 trilioni zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo na Sh. 114.74 bilioni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
“Fedha za matumizi yakKawaida zilizotengwa zinajumuisha Sh. 86.66 bilioni kwa ajili ya mishahara ya watumishi na Sh. 28.08 bilioni kwa ajili ya matumizi mengineyo. Vilevile, fedha za miradi ya maendeleo zilizotengwa zinajumuisha Sh. 2.52 trilioni ni fedha za ndani na Sh. 90.56 bilioni ni fedha za nje,” amesema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa ametaja miradi ya maendeleo iliyopewa kipaumbele katika bajeti ijayo ni ujenzi wa viwanja vya ndege, uboreshaji wa usalama wa usafiri katika Ziwa Victoria, Bandari ya Dar es Salaam, ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR), ukarabati wa Reli ya Tazara na mradi wa uboreshaji Kampuni ya NdegeTanzania (ATCL).
Leave a comment