Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184
AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184 za ngazi ya halmashauri, ili kuhakikisha inasogeza karibu huduma za bora za afya kwa wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa…(endelea).

Uzinduzi huo umefanyika leo tarehe 6 Mei 2024, katika Hospitali ya Wilaya ya Iringa Mjini (Frelimo), mkoani Iringa.

Akizungumza wakati anazindua mpango huo, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amesema zoezi hilo litaenda sambamba na usambazaji wa madaktari bingwa waliopewa jina la madaktari wa Rais Samia Suluhu Hassan, katika hospitali husika ili kuwapa uzoefu watoa huduma wake.

“Tumewaletea jopo nzuri sana la madaktari bingwa wa Rais Samia ili kuleta huduma za kibingwa na bobezi karibu na wananchi na azma kubwa ni kuboresha huduma za afya nchini,” amesema Ummy.

Ummy amesema lengo la madaktari bingwa hao kusambazwa katika hospitali za halmashauriu ni kuwajengea uwezo watoa huduma katika maeneo yao ya kazi ili kuimarisha utambuzi wa magonjwa, matibabu ya wagonjwa, upasuaji pamoja na rufaa kwa wagonjwa wa ngazi ya hospitali ya halmashauri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Afya

Kambi ya matibabu ya kibingwa Ruangwa yaacha vilio, DC atoa ombi JAI

Spread the loveMKUU wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma amefunga rasmi kambi...

error: Content is protected !!