Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi
ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the love

SERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo vikuu na vyuo vya ufundi stadi ili kuzifanyia maboresho kwa lengo la kuhakikisha wahitimu wake wanapata elimu bora itakayowawezesha nchi kupata rasilimali watu yenye ujuzi na maarifa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamebainishwa leo tarehe 7 Mei 2024, bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolph Mkenda, akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha wa 2024/25.

Prof. Mkenda amesema katika utekelezaji wa bajeti ya wizara yake ya 2024/25, watafanya mapitio ya mitaala 171, kuandaa mitaala mipya 18 pamoja na kuanzisha program za vipaumbele 145 za elimu ya juu. Pia, itaanzisha vituo vya elimu huruia ili kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu ya juu.

Katika hatua nyingine, Prof. Mkenda amesema wizara yake itahakiki mitaala 230 ya vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi, ili kuhakikisha mafunzo yanayotolewa yanakidhi mipango ya nchi, soko la ajira la kitaifa na kimataifa na kuwawezesha wahitimu kujiajiri na kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira.

“Serikali itaendelea na mapitio ya Sheria ya Elimu ili iendane na Sera ya Elimu na Mfunzo 2014 toleo la 2023. Vilevile itafanya mapitio ya sheria na miundo ya taasisi mbalimbali ikiwemo COSTECH, TLSB, NECTA, VETA, TCU, NACTVET na TEA ili ziendane na maboresho ya sera na sheria na makubaliano mbalimbali ya kikanda na kimataifa,” amesema Prof. Mkenda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!