Sunday , 19 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu
ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the love

SERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu, wenye sifa na uhitaji, kutoka 223,201 waliopata kwenye mwaka wa fedha wa 2023/24, hadi kufikia 252,243 watakaopewa 2024/25. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo, leo Jumanne bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema wanafunzi 84,500 wa mwaka wa kwanza ni miongoni mwa wanufaika wa mikopo hiyo inayotolewa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELSB).

“Wizara itaendelea kukusanya madeni ya mikopo iliyoiva ya kiasi cha Sh. 198 bilioni kutoka sekta ya umma na kuimarisha makusanyo kutoka sekta binafsi na isiyo rasmi. Aidha, itatafuta wanufaika wapya 40,000 wenye marejesho ya mikopo iliyoiva ikijumuisha wanufaika 5,000 wenye mikopo chechefu kutoka sekta binafsi na isiyo rasmi,” amesema Prof. Mkenda.

Kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu kwa 2024/25, Prof. Mkenda amesema wizara yake imepanga kutumia Sh. 1.96 trilioni, ikiwa ni ongezeko ikilinganishwa na bajeti ya Sh. 1.67 trilioni, iliyopitishwa na Bunge 2023/24.

Prof. Mkenda amesema, Sh. 1.32 trilioni zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo na Sh. 637 bilioni zimetengwa kwa ajili ya matumizi ya kaiwada ya wizara.

Waziri huyo wa elimu ametaja vipaumbele vya wizara yake kwa 2024/25, ikiwemo kuboresha elimu ya msingi, sekondari, vyuo vikuu na vya mafunzo ya ufundi stadi.

Prof. Mkenda amesema katika bajeti hiyo wizara yake itaongeza fursa na kuimarisha ubora wa mafunzo ya ufundi na ufundi stadi, kwa kuwezesha ujenzi wa shule mpya 100 za sekondari za ufundi, ambapo 26 zitaanza kupokea wanafunzi kuanzia Januari 2025. Pia, itaendelea na ujenzi wa vyuo vya mafunzo ya ufundi stadi 65.

“Wizara itaanzisha mafunzo ya ualimu katika vyuo vitatu vya VETA, Moshi, Dar es Salaam na Kagera, kwa lengo la kuongeza idadi ya walimu wenye sifa na ujuzi wa kufundisha vyuo vya elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi,” amesema Prof. Mkenda.

Katika hatua nyingine, Prof. Mkenda amesema mikopo ya elimu itatolewa kwa wanafunzi wa stashahada takribani 10,000 katika fani za kipaumbele na zenye uhaba wa watalaamu nchini ikiwamo fani za sayansi na ufundi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!