Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma
Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the love

NAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo yanayotolewa na Shirika la Amend kwa udhamini wa Ubalozi wa Uswis kwa madereva bodaboda 395 kwani yatawalinda raia wanaowabeba kwa ajili ya kujenga uchumi wa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza wakati wa kuhimishwa kwa mafunzo ya awamu ya pili ya usalama barabarani kwa Jiji la Dodoma ,Naibu Meya Asma Karama amesema kupita mafunzo hayo wanaamini ajali za barabarani zitapungua na ni vema bodaboda wanaendelea kuheshimu sheria za usalama barabarani.

Naibu Meya Asma amewasisitiza mafunzo hayo yawe chachu kwa bodaboda kuzingatia sheria na alama zilizopo  barabarani.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la Amend  Tanzania,  Simon Kalolo amesema mafunzo hayo yalianza Novemba 2023 kwa awamu ya kwanza na baadae kuja na awamu ya pili ya mafunzo ambayo yamehitimisha tarehe 5 Mei 2024 kwa waliopata mafunzo kukabidhiwa vyeti kutambua ushiriki wao.

Amesema pamoja na hayo mafunzo ya usalama barabarani ambayo wamekuwa wakiyatoa yanalenga pia kuunga mkono juhudi za Serikali katika kutokomeza ajali za barabarani nchini.

Wakati huo huo Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi Kikosi cha usalama barabarani jijini Dodoma, Tamim Songoro amesema mafunzo hayo yamekuwa na faida kwani yamesaidia kwa kiasi kikubwa maofisa usafirishaji(bodaboda)kujitambua na kupunguza ajali za mara kwa mara.

Kwa upande wa baadhi ya madereva bodaboda waliopatiwa mafunzo hayo wameshukuru Ubalozi wa Uswisi kwa kufanikisha mafunzo hayo na kuahidi watakuwa mabalozi wazuri kwa kufuata sheria za usalama barabarani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!