Rais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu kuanzia kesho Ijumaa kutokana na kifo cha Mkuu wa Majeshi nchini hiyo CDF- Francis Ogolla. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).
CDF Ogolla amefariki dunia leo Alhamis katika ajali ya helkopta ya jeshi la nchi hiyo iliyoanguka na kushika moto katika eneo la Sindar, lokesheni ya Kaben kwenye mpaka wa kaunti ya Elgeyo Marakwet na Pokot Magharibi nchini humo.
Ndege hiyo iliyokuwa na watu nane, watano wamefariki dunia papo hapo akiwamo mkuu huyo wa majeshi huku wengine watatu wakiripotiwa kupata majeraha.
Akihutubia taifa la Kenya leo jioni Rais Ruto amesema maomboleza hayo yataanza kesho tarehe 19 Aprili ikiwa ni pamoja na bendera kupepea nusu mlingoti.
Awali Kamanda wa Kaunti, Peter Mulinge alisema ndege hiyo ilianguka muda wa saa 8:50 mchana.
Ndege hiyo ilikuwa miongoni mwa zingine tatu na ilikuwa inaondoka eneo la Cheptulel Pokot Magharibi na ilikuwa ya kwanza kupaa, kabla ya kuanguka dakika chache baadaye.
Leave a comment