MWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge mkono chama chake cha zamani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), katika Uchaguzi Mkuu wa 2025 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Dk. Slaa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chadema, ametoa wito huo leo Jumatatu, akizungumza kwa njia ya simu katika mkutano wa hadhara wa Makamu mwenyekiti wa chama hicho bara, Tundu Lissu, uliofanyika jijini Dodoma.
Mwanasiasa huyo amesema, Chadema ndiyo chama pekee cha upinzani kinachoonyesha dhamira ya kutatua matatizo yanayowakabili wananchi.
“Ninawaomba watanzania tuhakikisheni tunaungana na Chadema, tunawaondoa hawa ambao sasa hivi wameonesha nia ya uhakika kwamba hawako upande wa wananchi. Mfano mjamzito anaenda hospitali lazima alipie gharama, huyu mama analeta mtanzania mpya anaongeza idadi yetu kweli tunashindwa kumlipia? Mbona Rais anapanda ndege kila siku ana hela za kutosha?” amesema Dk. Slaa.
Leave a comment