Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA
Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the love

Rais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia viongozi pamoja na wageni mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika na kubainisha miradi ambayo Tanzania inashirikiana na Mfuko Maalum wa Benki ya Dunia ambao unatoa mikopo nafuu na misaada kwa nchi zinazoendelea (IDA), kuitekeleza. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa nchi mbalimbali baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika.

Mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta (KICC) Jijini Nairobi nchini Kenya, unalenga kuainisha vipaumbele vya nchi hizo ili viweze kuzingatiwa kwenye mzunguko wa 21 wa IDA.

Akifafanua kuhusu miradi hiyo amesema Tanzania inashirikiana na IDA katika miradi mikubwa na ya kimkakati 25 katika sekta za uchukuzi, maendeleo ya kijamii, nishati, elimu, maji na uboreshaji wa mifumo ya kikodi.

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan akifuatilia hutoba zilizokuwa zinawasilishwa kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika.

“Mojawapo ya miradi ambayo nchi yetu inashirikiana na IDA kuitekeleza ni ile inayolenga kupunguza msongamano na kuboresha barabara za Jiji la Dar es Salaam ikiwemo ujenzi wa Kijazi Interchange na njia za Mabasi ya Mwendokasi inayohudumia wakazi zaidi ya 200,000 kwa siku. Miradi hii inachangia kwa kiasi kikubwa kubadili hali ya jiji la Dar es Salaam, hasa kiuchumi,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!