Thursday , 16 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni
Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Waziri wa Mali Asili na Utalii, Dk. Pindi Chana
Spread the love

 

WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka wa fedha wa 2024/25 ya kiasi cha Sh. 441.2 bilioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ombi hilo limewasilishwa bungeni jijini Dodoma, leo tarehe 29 Aprili 2024 na Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Pindi Chana, wakati akiwasilisha mpango na makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2024/25.

Balozi Chana amesema kiasi cha Sh. 112.4 bilioni zimetengwa kwa ajili ya mishahara ya watumishi, wakati Sh. 223.1 bilioni zikitengwa kwa ajili ya matumizi mengineyo na Sh. 105.6 bilioni zimepangwa kutumika kwenye miradi ya maendeleo.

Balozi Chana amewasilisha vipaumbele zaidi ya 15 vinavyotarajiwa kutekelezwa na wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha, ikiwemo utungaji wa Sera ya Taifa ya Haki Jinai, kushughulikia masuala ya kikatiba ikiwemo utoaji elimu ya katiba na uraia kwa umma. Kusimamia mfumo wa haki na utoaji haki na kuimarisha miundombinu ya mahakama.

Vipaumbele vingine ni kuharakisha mashauri ya kawaida na kumaliza mashauri ya muda mrefu, uandishi wa sheria na kuimarisha marejeo na ufuatiliaji wa utekelezaji mikataba iliyosainiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kupitia upya tozo za madini zinazotozwa na halmashauri

Spread the loveSERIKALI inaendelea na zoezi la kupitia tozo na ushuru wa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge CCM aibana Serikali ukamilishaji miradi kwa bajeti inayofikia ukingoni

Spread the loveMBUNGE wa Hai (CCM), mkoani Kilimanjaro, Saashisha Mafuwe, ameibana Serikali...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Hatuoni faida ya demokrasia

Spread the loveMwenyekiti wa Chadema, Fremaan Mbowe amesema Tanzania haijanufaika na miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ataka wananchi wasiruhusu bakora za Magufuli

Spread the loveMwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Profesa Ibrahimu Lipumba...

error: Content is protected !!