Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi
Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the love

RAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri, kuwa Mkuu wa Majeshi (CDF)wa taifa hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Kenya, Jenerali Kahariri ambaye kabla ya kupandishwa cheo alikuwa Luteni Jenerali, ameteuliwa kushika wadhifa huo leo tarehe 2 Mei 2024, akichukua mikoba ya Jenerali Francis Ogolla, aliyefariki dunia kwa ajali ya chopa (helkopta).

Jenerali Kahariri pia aliwahi kuwa Makamu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi. Baada ya Jenerali Ogolla kufariki dunia, aliteuliwa kukaimu kwa muda nafasi hiyo hadi alipoteuliwa rasmi na Rais Ruto.

“Rais Ruto leo amempandisha cheo Luteni Jenerali Charles Muriu Kahariri hadi cheo cha Jenerali na kumteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi.,” imesema taarifa ya Ikulu ya Kenya.

Katika hatua nyingine, Rais Ruto amemteua Meja Jenerali John Omenda, kuwa Makamu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, wakati Meja Jenerali Fatuma Gaiti akiteuliwa kuwa Kamanda wa Jeshi la Anga la Kenya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!