Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari Aliyesomeshwa na mchumba aamuriwa kurudisha Sh 9.4 Mil. baada ya kukataa kuolewa
HabariKimataifa

Aliyesomeshwa na mchumba aamuriwa kurudisha Sh 9.4 Mil. baada ya kukataa kuolewa

Spread the love

 

MWANAMKE mmoja nchini Uganda ambaye aliuumiza moyo wa mchumba wake ameamrishwa na mahakama kulipia hasara za kifedha kwa uchungu wa kisaikolojia. Yameripoti Mashirika ya Kimataifa.

BBC imeandika kuwa Mahakama ya Kanungu ilisema kuwa Richard Tumwine alilipa Sh 9.4 milioni kwa ajili ya masomo ya sheria ya Fortunate Kyarikunda, pesa ambazo sasa atatakiwa kuzilipa pamoja na gharama za kesi.

Kwa kusitisha uchumba wao baada ya miaka minne, Hakimu Asanasio Mukobi aliamua kuwa Kyarikunda alikiuka ahadi na kusababisha madhara kwa Tumwine.

Mahakama ilisema kuwa ni “isiyo na maana, upotoshaji na ulaghai” kwa mshitakiwa kudai kuwa wazazi wake walimwambia asiolewe na mwanaume mzee sana, ikisema” alikuwa na wakati wote wa kukataa maombi ya mapenzi mapema na kuepuka kutumia pesa zake “.

Haijulikani iwapo Kyarikunda atakata rufaa dhidi ya hukumu.

Wakosoaji wanasema gazeti la Monitor kwamba hukumu ina kasoro kwasababu uchumba ni tofauti na ndoa ambayo inakubalika kisheria.

Wakati huo huo Sheila Kawamara, kutoka kikundi cha utetezi wa wanawake ED EASSI, anaonya kuwa wakati mwingine huwa kuna hali za unyonyaji ambapo mwanaume humpatia pesa mwanamke kwa sharti kuwa atamuoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!