Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari Aliyesomeshwa na mchumba aamuriwa kurudisha Sh 9.4 Mil. baada ya kukataa kuolewa
HabariKimataifa

Aliyesomeshwa na mchumba aamuriwa kurudisha Sh 9.4 Mil. baada ya kukataa kuolewa

Spread the love

 

MWANAMKE mmoja nchini Uganda ambaye aliuumiza moyo wa mchumba wake ameamrishwa na mahakama kulipia hasara za kifedha kwa uchungu wa kisaikolojia. Yameripoti Mashirika ya Kimataifa.

BBC imeandika kuwa Mahakama ya Kanungu ilisema kuwa Richard Tumwine alilipa Sh 9.4 milioni kwa ajili ya masomo ya sheria ya Fortunate Kyarikunda, pesa ambazo sasa atatakiwa kuzilipa pamoja na gharama za kesi.

Kwa kusitisha uchumba wao baada ya miaka minne, Hakimu Asanasio Mukobi aliamua kuwa Kyarikunda alikiuka ahadi na kusababisha madhara kwa Tumwine.

Mahakama ilisema kuwa ni “isiyo na maana, upotoshaji na ulaghai” kwa mshitakiwa kudai kuwa wazazi wake walimwambia asiolewe na mwanaume mzee sana, ikisema” alikuwa na wakati wote wa kukataa maombi ya mapenzi mapema na kuepuka kutumia pesa zake “.

Haijulikani iwapo Kyarikunda atakata rufaa dhidi ya hukumu.

Wakosoaji wanasema gazeti la Monitor kwamba hukumu ina kasoro kwasababu uchumba ni tofauti na ndoa ambayo inakubalika kisheria.

Wakati huo huo Sheila Kawamara, kutoka kikundi cha utetezi wa wanawake ED EASSI, anaonya kuwa wakati mwingine huwa kuna hali za unyonyaji ambapo mwanaume humpatia pesa mwanamke kwa sharti kuwa atamuoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Kimataifa

Tanzania, Italia kuimarisha ushirikiano sekta za kimkakati

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania na Italia zimeahidi kuimarisha ushirikiano katika...

Habari za SiasaKimataifa

Odinga avuka kihunzi cha kwanza uenyekiti AUC

Spread the loveAZMA ya kiongozi wa Azimio La Umoja-One Kenya, Raila Odinga...

Kimataifa

‘Wachawi’ 50 wafariki baada ya kumeza dawa mitishamba

Spread the loveWatu zaidi ya 50 wanaoshutumiwa kwa ‘uchawi’ wamefariki dunia nchini...

error: Content is protected !!