Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Majaji kuamua hatima ya Zuma leo
Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the love

Majaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa zamani wa nchi hiyo, Jacob Zuma ataruhusiwa kugombea kwenye uchaguzi wa Mei mwaka huu. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Zuma ambaye anawania kwa tiketi ya chama cha upinzani, alikata rufaa dhidi ya uamuzi wa maafisa wa tume ya uchaguzi waliomkatalia kugombea kutokana na kupatikana na hatia mwaka 2021.

Jana Jumatatu, Zuma mwenye umri wa miaka 81 alikuwa mahakamani mjini Johannesburg wakati mawakili wakijadi kesi hiyo.

“Ikiwa raia wanataka niwe rais, nani atawazuia?”, Zuma aliwambia wafuasi wake baada ya kesi kusikilizwa. “Niruhusu niende na nimalizie kile nilichokianza.”

Afrika Kusini inafanya uchaguzi mkuu tarehe 29 Mei ambao unatarajiwa kuwa uchaguzi wenye ushindani mkali tangu ujio wa demokrasia mwaka 1994.

Chama tawala cha African National Congress kinakabiliwa na changamoto katika kura ya maoni na kuna hatari kipoteza wingi wa wabunge tangu kumalizika kwa utawala wa kibaguzi, kutokana na uchumi dhaifu na madai ya ufisadi na usimamizi mbaya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!