Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watu 30 mbaroni tuhuma kughushi nyaraka za mafao kupata fedha NSSF
Habari Mchanganyiko

Watu 30 mbaroni tuhuma kughushi nyaraka za mafao kupata fedha NSSF

Spread the love

WATU 30 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kwa tuhuma za kughushi nyaraka za mafao ili kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu katika Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 9 Aprili 2024 na Kamanda wa Jeshi la Polisi wa kanda hiyo, SACP Jumanne Muliro, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kamanda Muliro amesema polisi walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao kwa kushirikiana na maafisa kutoka NSSF.

Amesema watafikishwa mahakamani kwa makosa ya kujihusisha na mambo ya kughushi nyaraka mbalimbali na kupanga mpango wa kuliibia shirika hilo.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na maofisa kutoka NSSF limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 30, wanaotuhumiwa kughushi nyaraka mbalimbali zinazohusiana na mafao ya mfuko huo kwa lengo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu,” amesema Kamanda Muliro na kuongeza:

“Sehemu ya ushahidi imepatikana na watafikishwa mahakamani kwa kosa la kujihusisha na mambo ya kughushi nyaraka mbalimbali na kupanga mpango wa kuliibia shirika hilo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!