Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa
Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the love

Spika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu wadhifa wake huku kukiwa na uchunguzi wa tuhuma za rushwa wakati akiwa waziri wa ulinzi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hayo yanajiri baada ya wiki iliyopita nyumba ya Spika huyo kuvamiwa na maofisa upelelezi, ikiwa ni sehemu ya uchunguzi wa tuhuma hizo za rushwa.

Akitangaza kujiuzulu jana Jumatano, Mapisa-Nqakula alisema; “Kujiuzulu kwangu sio dalili au kukubali hatia kuhusiana na tuhuma zinazotolewa dhidi yangu.”

Kujiuzulu huko, ambako kunaanza kutekelezwa mara moja, pia kunaambatana naye kuacha kazi kama mbunge.

Mapisa-Nqakula alikuwa waziri wa ulinzi nchini humo kuanzia mwaka 2012 hadi 2021.

Shirika la utangazaji la serikali ya Afrika Kusini (SABC) liliripoti kwamba anatuhumiwa kupokea mamilioni ya pesa taslimu kama hongo kutoka kwa wakandarasi wa zamani wa kijeshi.

Mapisa-Nqakula alichukua likizo maalum baada ya uvamizi huo na juzi Jumanne, ombi lake kwa mahakama kuzuia mamlaka kumkamata, lilitupiliwa mbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

error: Content is protected !!