Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mnyika aacha ujumbe msibani kwa kada wa Chadema aliyefia vitani Ukraine
Habari

Mnyika aacha ujumbe msibani kwa kada wa Chadema aliyefia vitani Ukraine

Spread the love

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-Chadema Taifa, John Mnyika mapema leo amefika msibani nyumbani kwa kada wa chama hicho aliyefia vitani nchini Ukraine akiipigania Urusi, Nemes Tarimo na kuacha ujumbe. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Katika ujumbe wake Mnyika ameonesha namna chama chake kinavyotambua mchango wa Nemes katika mapambano ya haki, demokrasia na maendeleo ya wananchi.

“Rest in peace mpambanaji Nemes Raymond Tarimo, nilipokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo chako, umetangulia mbele za haki katika umri mdogo. Tukiwa bado tunatamani mchango wako katika mapambano ya kutafuta uhuru, haki, demokrasia na maendeleo ya watu Chadema katika jimbo la Kibamba linatambua mchango wako wakati wa mchakato wa kura za maoni ya uteuzi wa mgombea ubunge jimbo la Kibamba katika uchaguzi wa mwaka 2020 ni sala yangu kuwa Mwenyezi Mungu akupe rehema na neema ya kupata mwanga wa milele. Upumzike kwa Amani,” ameandika nyika katika kitabu hicho.

Naye Mwenyekiti wa Chadema kata ya Saranga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bawacha mkoa wa Ubungo, Magreth Kyai, amesema msiba huo umewagusa sana kwasababu Nemes alikuwa mtu wa karibu mwenye kujali wanachama, alipenda siasa na alipenda chama chake cha Chadema.

Amesema ushiriki wa Chama katika msiba huo ni kubwa kwani Katibu Mkuu amefika na kutoa ujumbe na pia viongozi wa chama mkoa wa Ubungo watafika na wametoa rambirambi zao kama chama.
Mwili wa Nemes umewasili leo kutokea nchini Urusi na utaagwa nyumbani kwake Saranga na baadae kusafirsihwa kwenda mkoani Mbeya kwa maziko

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Habari

Tanzania yaungana na nchi 180 kushiriki maonesho ya utalii Ujerumani

Spread the love  TANZANIA imeungana na mataifa 180 duniani kushiriki maonesho makubwa...

error: Content is protected !!