Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi yakana kupandisha gharama za maisha duniani
Kimataifa

Urusi yakana kupandisha gharama za maisha duniani

Rais wa Urusi, Vladimir Putin
Spread the love

 

WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Urusi, Sergey Lavrov amesisitiza kwamba nchi hiyo haihusiki kwa vyovyote vile na ongezeko la bei ya bidhaa muhimu duniani.

Ameongeza kwamba taarifa hizo zinaenezwa na nchi za Magharibi ili kueneza chuki dhidi ya nchi hiyo. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Waziri huyo ametoa kauli hiyo leo tarehe 27 Julai jiiini Kampala, Uganda ambako yupo kwenye ziara yake ya nchi nne za Afrika.

Uganda ni nchi ya tatu kwenye ziara yake Afrika.

Sergey Lavrov amesisitiza kwamba Urusi haihusiki kwa vyovyote na ukosefu wa nafaka, ngano, mafuta na kupanda kwa gharama ya maisha kote duniani, kama inavyoripotiwa kutokana na uvamizi wake nchini Ukraine.

Lavrov amedai kwamba mataifa ya Magharibi yamekuwa na hulka ya kuilaumu Urusi kwa kila baya.

Amesema gharama ya maisha zilianza kupanda kabla ya vita vya Ukraine, kwani zilianza katika kipindi cha janga la virusi vya Corona.

Licha ya kudai kwamba Urusi haihusiki na hali mbaya ya uchumi duniani, amedai kwamba vikwazo vya mataifa ya Magharibi dhidi ya Urusi ndiyo vimechangia hali hiyo, kwa kuvuruga usafirishaji wa
bidhaa muhimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!