Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ujerumani yamchunguza anayedaiwa kuwa jasusi la Uturuki
Kimataifa

Ujerumani yamchunguza anayedaiwa kuwa jasusi la Uturuki

Angela Merkel
Spread the love

 

MWENDESHA mashitaka nchini Ujerumani, ameanza uchunguzi dhidi ya raia mmoja wa Uturuki, anayetuhumiwa kwa ujasusi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu nchini humo imesema, inamchunguza mtu aliyekamatwa wiki mbili zilizopita kwa madai ya kufanya ujasusi kwa niaba ya idara ya kijasusi ya Uturuki.

Mtuhumiwa huyo alikamatwa katika mji wa Dusseldorf.

Msemaji wa mamlaka hiyo yenye makao yake mjini Karlsruhe, ameliambia shirika la habari la Ujerumani (DPA), kulikuwa na ushahidi wa kutosha unaoshiria mtu huyo alikusanya taarifa kuhusiana na wafuasi wa kile kinachoitwa vuguvugu la Gulen katika eneo la Köln.

Uturuki inamlaumu kiongozi wa kidini anayeishi Marekani, Fethullah Gulen kwa kuandaa jaribio la mapinduzi la 15 Julai 2016, lililoshindwa.

Mamlaka za Ujerumani zilimkamata mtu huyo tarehe 27 Septemba katika operesheni pana ya kipolisi na baadaye idara ya masuala ya dharura ziling’amua nyaraka zilizoashiria kitisho kwa baadhi ya watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!