UKISTAAJABU ya Mussa uyataona ya Firauni. Ndivyo unavyoweza kuelezea kile alichokifanya Khoirul Anam, raia wa Indonesia aliyeamua kufunga ‘ndoa’ na ‘rice cooker.’ Anaripoti Mitanga Hunda, TUDARCo … (endelea).
Unaweza fikiria ni simulizi, lahasha ni kweli mwanaume huyo ameamua kufunga pingu za maisha na kifaa hicho cha kupikia na picha zake kuibua mjadaa.
Picha ndoa hizo, amezeweka wiki mbili zilizopika katika ukurasa wake wa facebook na kuibua mjadala wa namna gani hicho alichokifanya kinashangaza.
Yeye pamoja na ‘mke wake’ huyo ambaye ni rice cooker walivalia mavazi meupe na akionekana kuibusha rice cooker hiyo ambayo ilifunikwa kwa shera mithili ya bibi harusi.
Picha hizo alizoweka kwenye facebook, zilikwenda sambamba na maneno akisema, nyeupe, nyeupe, nyeupe, mwenye upendo. Sina maneno mengi ya kusema. Mimi ni mahiri wa kupika.
Bila wewe mchele wangu siwezi kuupika. Akaweka emoji za kucheka na kumalizia akisema burudani.
Nomaaa