Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kiongozi wa kijeshi wa Guinea kuapishwa kuwa rais
Kimataifa

Kiongozi wa kijeshi wa Guinea kuapishwa kuwa rais

Kanali Mamady Doumbouya (katikati)
Spread the love

 

KIONGOZI wa kijeshi nchini Guinea, Kanali Mamady Doumbouya anatarajiwa kuapishwa leo tarehe 1 Oktoba 2021kama rais wa mpito. Anaripoti Patricia Kighono, TUDARCo … (endelea).

Sherehe ya kuapishwa kwake itafanyika katika ikulu ya rais na kuhudhuriwa na watu walioalikwa pekee.

Kanali Doumbouya aliongoza mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Rais Alpha Condé mapema mwezi uliopita.

Kiongozi huyo wa kijeshi mwenye umri wa miaka 41, anatarajiwa kuunda serikali katika wiki chache zijazo.

Doumbouya atakuwa kiongozi wa pili wa Barani Afrika mwenye umri mdogo kuongoza nchi, mdogo zaidi akiwa ni wa Mali, Kanali Assimi Goïta (38) ambaye aliongoza mapinduzi ya kumng’oa madarakani Rais Ibrahim Keïta.

Baada ya mapinduzi ya Guinea, Kanali Doumbouya alisema askari wake wamechukua uongozi na walimedhamiri kumaliza ufisadi, ukiukwaji wa haki za binadamu na usimamizi mbaya uliokithiri nchini humo.

Rais Condé alichaguliwa katika uchaguzi uliokumbwa na utata kuongoza kwa muhula wa tatu licha ya maandamano ya ghasia mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!