Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kiongozi wa kijeshi wa Guinea kuapishwa kuwa rais
Kimataifa

Kiongozi wa kijeshi wa Guinea kuapishwa kuwa rais

Kanali Mamady Doumbouya (katikati)
Spread the love

 

KIONGOZI wa kijeshi nchini Guinea, Kanali Mamady Doumbouya anatarajiwa kuapishwa leo tarehe 1 Oktoba 2021kama rais wa mpito. Anaripoti Patricia Kighono, TUDARCo … (endelea).

Sherehe ya kuapishwa kwake itafanyika katika ikulu ya rais na kuhudhuriwa na watu walioalikwa pekee.

Kanali Doumbouya aliongoza mapinduzi yaliyomuondoa madarakani Rais Alpha Condé mapema mwezi uliopita.

Kiongozi huyo wa kijeshi mwenye umri wa miaka 41, anatarajiwa kuunda serikali katika wiki chache zijazo.

Doumbouya atakuwa kiongozi wa pili wa Barani Afrika mwenye umri mdogo kuongoza nchi, mdogo zaidi akiwa ni wa Mali, Kanali Assimi Goïta (38) ambaye aliongoza mapinduzi ya kumng’oa madarakani Rais Ibrahim Keïta.

Baada ya mapinduzi ya Guinea, Kanali Doumbouya alisema askari wake wamechukua uongozi na walimedhamiri kumaliza ufisadi, ukiukwaji wa haki za binadamu na usimamizi mbaya uliokithiri nchini humo.

Rais Condé alichaguliwa katika uchaguzi uliokumbwa na utata kuongoza kwa muhula wa tatu licha ya maandamano ya ghasia mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!