Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Watu wasiojulikana’ wavamia ofisi za gazeti waua watano
KimataifaTangulizi

‘Watu wasiojulikana’ wavamia ofisi za gazeti waua watano

Mfano wa mtu aliyefanya mashambulizi katika Chumba cha habari cha gazeti la Capital Gazette la Marekani. Picha ndogo ofisi za gazeti hilo
Spread the love

WATU wasiojulikana wamevamia ofisi za gazeti la Capital Gazette na kufyatua risasi na kuua watu watano na kuwajeruhi wengine, katika jiji la Maryland, Marekani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mmoja wa wafanyakazi wa gazeti hilo amesema kuwa mtu aliyefyatua risasi katika chumba cha habari kupitia kwenye dirisha la vioo.

“Tukiwa kwenye madawati yetu katika chumba cha habari, tulistuka kusikia mtu akikoki bunduki na ghafla kuanza kusikia milio la risasi. Ni tukio la kustiha sana sana.” Aliandika mmoja ya waandishi walionusurika, Phil Davis katika ukurasa wake wa Twitter.

Polisi wameimarisha ulinzi katika eneo hilo na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

“Hili ni tukio baya sana lililotokea mchana huu,” alisema Mtendaji wa eneo hilo, Steve Schuh katika mkutano na waandishi wa habari. “Watu kadhaa wamefariki katika tukio hilo.”

Polisi wamesema kwa sasa hawawezi kutambua hasa ni aina gani ya silaha iliyotumika, lakini uchunguzi unaendelea wakisaidia na FBI na taasisi nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

error: Content is protected !!