WAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya mikoa ya ukanda wa Pwani ikiwamo Lindi, Mtwara, Pwani na Dar es Salaam, tayari baadhi ya wakazi wa kisiwa cha Mafia mkoani Pwani wamepoteza makazi yao kutokana na athari ya kimbuga Hidaya kilichotokea jana Ijumaa usiku. Anaripoti Faki Sosi… (endelea).
Kimbunga hicho kilichokadiriwa kulichoambatana na mvua kubwa, kimeezua paa za nyumba za wakazi wa kisiwa hicho, huku nyumba nyingine zikivunjika kwa kudondokewa na miti ya minazi na miembe.
Taarifa za awali kutoka kwa wakazi hao, zinasema kimbunga hicho kimeleta athari kubwa kwa wakazi wa Kata za Jibondo, Kiegeani na Kilindoni.
Hali ilivyo asubuhi hii katika baadhi ya maeneo ya kisiwani Mafia mkoani Pwani, ambapo miti imeng’oka na kuangukia nyumba, huku baadhi ya mapaa ya nyumba yaking’oka kutokana na upepo mkali uliosababishwa na Kimbunga Hidaya kinachoendelea kukaribia katika Pwani ya Bahari ya Hindi pic.twitter.com/OrtvwGTdF9
— MwanaHALISI Digital (@Mwanahalisitz) May 4, 2024
Akizungumzia hali hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Sauda Mangosongo ameieleza MwanaHALISI Online kuwa tayari timu yake ya usalama ipo kwenye sehemu yalipotokea maafa hayo hivyo baadaye atatoa taarifa juu juu ya tukio hilo.
Leave a comment