Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Watu wasiojulikana’ wavamia ofisi za gazeti waua watano
KimataifaTangulizi

‘Watu wasiojulikana’ wavamia ofisi za gazeti waua watano

Mfano wa mtu aliyefanya mashambulizi katika Chumba cha habari cha gazeti la Capital Gazette la Marekani. Picha ndogo ofisi za gazeti hilo
Spread the love

WATU wasiojulikana wamevamia ofisi za gazeti la Capital Gazette na kufyatua risasi na kuua watu watano na kuwajeruhi wengine, katika jiji la Maryland, Marekani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mmoja wa wafanyakazi wa gazeti hilo amesema kuwa mtu aliyefyatua risasi katika chumba cha habari kupitia kwenye dirisha la vioo.

“Tukiwa kwenye madawati yetu katika chumba cha habari, tulistuka kusikia mtu akikoki bunduki na ghafla kuanza kusikia milio la risasi. Ni tukio la kustiha sana sana.” Aliandika mmoja ya waandishi walionusurika, Phil Davis katika ukurasa wake wa Twitter.

Polisi wameimarisha ulinzi katika eneo hilo na uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

“Hili ni tukio baya sana lililotokea mchana huu,” alisema Mtendaji wa eneo hilo, Steve Schuh katika mkutano na waandishi wa habari. “Watu kadhaa wamefariki katika tukio hilo.”

Polisi wamesema kwa sasa hawawezi kutambua hasa ni aina gani ya silaha iliyotumika, lakini uchunguzi unaendelea wakisaidia na FBI na taasisi nyingine.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!