Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Amnesty International: Burundi si shwari
Kimataifa

Amnesty International: Burundi si shwari

Mji wa Bujumbura
Spread the love

SHIRIKA la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa ripoti inayoonyesha hali ya usalama kutokuwa shwari nchini Burundi, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa ya Shirika hilo imesema kwamba nchi hiyo imekuwa ikikabiliwa na vitendo vya mateso, watu kufungwa bila makosa, kubakwa na hata kuuwawa.

Shirika hilo limetoa tahadhari kwa umoja wa mataifa kufikiria kwa kina kuhuzu wakimbizi wanaorejea Burundi kutoka Tanzania kwa kuwa wengi wapo katika hatari za kiusalama nchini mwao.

Mwezi uliopita, Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi (UNHCR) walikubaliana kwamba kufikia mwisho wa mwaka huu wawe wamewarejesha wakimbizi 12,000 wanaoishi Tanzania wanaotaka kurudi kwao kwa hiari.

Shirika la Amnesty International linasema, mpango huu unahatarisha maisha ya maelfu ya wakimbizi na linaamini kuwa wakimbizi wengi wanarejeshwa nyumbani kwao kutokana na msukumo wa ushawishi kutoka serikali ya Tanzania na Burundi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!