Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Serikali ya Magufuli yalitia ‘kitanzi’ Raia Mwema
Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali ya Magufuli yalitia ‘kitanzi’ Raia Mwema

Dk. Hassan Abbas, Mkurugenzi wa Idara Habari Maelezo. Picha ndogo toleo la gazeti Raia Mwema lililosababisha kufungiwa
Spread the love

UHURU wa vyombo vya habari hususani magazeti umezidi   kuwa mashakani baada ya leo serikali kutangaza kulifungia gazeti linalotolewa kilawiki la Raia mwema, anaandika Faki Sosi.

Gazeti hilo lilianzishwa na kumilikiwa na waandishi wa habari wakongwe na jana limefungiwa katika kipindi cha miezi mitatu.

Kufungwa kwa gazeti hilo kumekuja ikiwa imepita wiki moja tangu serikali ilipolifunga gazeti la MwanaHALISI linalomikiwa pia na Mwandishi,  Saed Kubenea.

Mkuregenzi wa Idara ya Habari (Maelezo), Dk.  Hassan Abbas ambaye pia ndiye msemaji wa Serikali leo ametangaza kulifungia gazeti hilo kwa  muda wa siku 90.

Wakati Rais Mwema likifungiwa miezi mitatu, MwanaHALISI limefungiwa miezi 24 miaka (miwili).

Mhariri wa gazeti hilo jana aliitwa na serikali kujieleza kwa nini alifungiwe kwa madi ya kuandika habari ya uchambuzi iliyobebwa na kichwa cha habari,  “Magufuli urais utamshinda”

Habari hiyo ilichapishwa katika gazeti hilo la Septemba 27 mwaka huu. Mhariri mtendaji wa gazeti hilo, Godfrey Dilunga amethibitisha kufungiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mikataba ya utekelezaji bado haijasainiwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

error: Content is protected !!