Friday , 9 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Amnesty International: Burundi si shwari
Kimataifa

Amnesty International: Burundi si shwari

Mji wa Bujumbura
Spread the love

SHIRIKA la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa ripoti inayoonyesha hali ya usalama kutokuwa shwari nchini Burundi, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa ya Shirika hilo imesema kwamba nchi hiyo imekuwa ikikabiliwa na vitendo vya mateso, watu kufungwa bila makosa, kubakwa na hata kuuwawa.

Shirika hilo limetoa tahadhari kwa umoja wa mataifa kufikiria kwa kina kuhuzu wakimbizi wanaorejea Burundi kutoka Tanzania kwa kuwa wengi wapo katika hatari za kiusalama nchini mwao.

Mwezi uliopita, Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi (UNHCR) walikubaliana kwamba kufikia mwisho wa mwaka huu wawe wamewarejesha wakimbizi 12,000 wanaoishi Tanzania wanaotaka kurudi kwao kwa hiari.

Shirika la Amnesty International linasema, mpango huu unahatarisha maisha ya maelfu ya wakimbizi na linaamini kuwa wakimbizi wengi wanarejeshwa nyumbani kwao kutokana na msukumo wa ushawishi kutoka serikali ya Tanzania na Burundi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Kagame afumua tena Jeshi, awafuta kazi maofisa zaidi ya 200 wakiwemo majenerali

Spread the love  RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amewafuta kazi Meja Jenerali...

Kimataifa

Urusi imelipua bwawa kuu la umeme nchini Ukraine

Spread the loveSERIKALI mjini Kyiv nchini, Ukraine imeushutumu utawala wa Rais Vladimir...

Kimataifa

Rais Kagame afanyia mabadiliko makubwa jeshi, usalama wa taifa

Spread the loveRAIS wa Rwanda, Paul Kagame amefanye uteuzi wa wakuu wapya...

Kimataifa

Miili ya waliofariki kwenye ajali ya treni India, kukabidhiwa baada ya vipimo vya DNA

Spread the love  TAKRIBANI watu 260 wamefariki na wengine karibu 650 wamejeruhiwa...

error: Content is protected !!