Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Amnesty International: Burundi si shwari
Kimataifa

Amnesty International: Burundi si shwari

Mji wa Bujumbura
Spread the love

SHIRIKA la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetoa ripoti inayoonyesha hali ya usalama kutokuwa shwari nchini Burundi, anaandika Mwandishi Wetu.

Taarifa ya Shirika hilo imesema kwamba nchi hiyo imekuwa ikikabiliwa na vitendo vya mateso, watu kufungwa bila makosa, kubakwa na hata kuuwawa.

Shirika hilo limetoa tahadhari kwa umoja wa mataifa kufikiria kwa kina kuhuzu wakimbizi wanaorejea Burundi kutoka Tanzania kwa kuwa wengi wapo katika hatari za kiusalama nchini mwao.

Mwezi uliopita, Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia wakimbizi (UNHCR) walikubaliana kwamba kufikia mwisho wa mwaka huu wawe wamewarejesha wakimbizi 12,000 wanaoishi Tanzania wanaotaka kurudi kwao kwa hiari.

Shirika la Amnesty International linasema, mpango huu unahatarisha maisha ya maelfu ya wakimbizi na linaamini kuwa wakimbizi wengi wanarejeshwa nyumbani kwao kutokana na msukumo wa ushawishi kutoka serikali ya Tanzania na Burundi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!