Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Libya atumbuliwa baada ya kukutana na mwenzie wa Israel
Kimataifa

Waziri Libya atumbuliwa baada ya kukutana na mwenzie wa Israel

Spread the love

KIONGOZI wa serikali ya Libya amemsimamisha kazi waziri wake wa mambo ya nje baada ya mwenzake wa Israel kutangaza kuwa, wawili hao walifanya mazungumzo mjini Rome wiki iliyopita. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea)

Waziri Mkuu, Abdulhamid Dbeibah amesema jana Jumapili katika taarifa iliyochapishwa pia kwenye mtandao wa Facebook kuwa Najla al-Mangoush amesimamishwa kazi kwa muda na atakuwa chini ya uchunguzi wa tume inayoongozwa na waziri wa sheria.

Wizara ya mambo ya nje ya Libya imeelezea kuwa mkutano huo ulikuwa sio rasmi na kwamba wawili hao walikutana bila kupanga, japo taarifa za mkutano huo tayari zimesababisha maandamano katika miji kadhaa ya Libya.

Mzozo huo wa kisiasa ulizuka jana jioni baada ya wizara ya mambo ya nje ya Israel kueleza kuwa, mawaziri wa mambo ya nje wa Israel na Misri walikutana wiki iliyopita.

Taarifa hiyo imeendelea kueleza kuwa, Waziri wa mambo ya nje wa Israel, Eli Cohen na Mangoush, mwenzake wa Libya, walizungumza mjini Rome katika mkutano ulioandaliwa na Waziri wa mambo ya nje wa Italia, Antonio Tajani.

Israel imeuelezea mkutano huo kama mpango wa kwanza wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.

Tangu mnamo mwaka 2020, Israel imekuwa ikijaribu kurejesha uhusiano wake na mataifa kadhaa ya Kiislamu kupitia mkataba maarufu kama Abraham Accords, uliosimamiwa na Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!