Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Mnangagwa ashinda uchaguzi, upinzani wapinga
Kimataifa

Rais Mnangagwa ashinda uchaguzi, upinzani wapinga

Spread the love

TUME ya taifa ya uchaguzi nchini Zimbabwe imemtangaza Rais Emmerson Mnangagwa kuwa mshindi wa kiti cha Urais katika uchaguzi uliofanyika Jumatano 23 Agosti 2023.

Hata hivyo, upinzani umeyakataa matokeo ya uchaguzi ambao waangalizi wa kimataifa walisema pia kuwa haukukidhi viwango vya demokrasia. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kulingana na matokeo rasmi yaliyotangazwa jana Jumapili na mwenyekiti wa Tume ya taifa ya uchaguzi ya nchi hiyo Justice Chigumba, Rais Emmerson Mnangagwa mwenye miaka 80, ameshinda kwa kupata asilimia 52.6 ya kura dhidi ya asilimia 44 za mpinzani wake mkuu Nelson Chamisa, mwenye miaka 45.

Katika uchaguzi huo, raia wa Zimbabwe walikwenda katika vituo vya kupigia kura kuchagua rais na wabunge Jumatano na Alhamisi, katika zoezi lililotawaliwa na ucheleweshaji kitendo ambacho kilichochea shutuma za udanganyifu na ukandamizaji wa wapigakura zilizotolewa na upinzani.

Matokeo ya uchaguzi wa Rais yalipokelewa kwa nderemo na wafuasi wachache wa chama tawala katika ukumbi wa mikutano, lakini msemaji wa chama cha “Citizens Coalition for Change” cha Nelson Chamisa alisema kuwa chama hicho hakikutia saini majumuisho ya mwisho aliyoyataja kuwa ya uongo.

Alisema kuwa hawawezi kuyakubali matokeo na kwamba hivi karibuni chama hicho kitatangaza hatua inayofuata.

Akijibu madai ya upinzani, Rais Mnangagwa amesema wanaohoji matokeo ya uchaguzi wanapaswa kwenda mahakamani.

Uchaguzi wa Zimbabwe ulikuwa ukitazamwa katika mataifa ya Kusini mwa Afrika kama kipimo cha uungwaji mkono wa chama cha Mnangagwa cha ZANU-PF ambacho utawala wake wa miaka 43 umekuwa ukikabiliwa na mdororo wa uchumi na tuhuma za uongozi wa kibabe.

Mwaka mmoja baadaye, alimshinda kwa tofauti ndogo Nelson Chamisa kwa mara ya kwanza katika uchaguzi ambao viongozi wa upinzani waliulaani kuwa ulikuwa na vitendo vya udanganyifu.

Uchaguzi wa wiki hii, ulilazimika kuingia katika siku ya pili kwa sababu ya kucheleweshwa kwa karatasi za kupigia kura katika baadhi ya maeneo muhimu ikiwemo Harare, ambapo ni ngome ya upinzani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!