RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ametahadharisha uwepo wa mfumuko mkubwa wa bei nchini unaosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta duniani kutokana na vita inayoendelea kati ya Ukraine na Urusi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Rais Samia ametoa tahadhari hiyo leo tarehe 8 Machi 2022, katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika viwanja vya Maisara Visiwani Zanzibar.
Mkuu huyo wa nchi amesema jinsi mafuta yanavyopanda bei, Tanzania haitanusurika kwani bidhaa zote zitapanda bei.
“Bidhaa zitapanda bei, nauli zitapanda bei, kila kitu kitapanda, thamani ya kila kitu itapanda kwasababu mafuta yanapanda bei,” amesema Rais Samia.
Aidha amesema kuna minong’ono imenza kusikika kuwa maisha yamekuwa magumu huku lawama zikipelekwa kwa viongozi kuwa hawana baraka.
“Si baraka ya kiongozi, ni hali ya ulimwengu inavyokwenda mafuta yanapanda bei duniani na bidhaa zote zitapanda bei,” amesisitiza.
Leave a comment