ALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa Mkulo amefariki dunia leo tarehe 4 Mei 2024 katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mke wa marehemu, Julie Mkulo msiba upo nyumbani kwa marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, taarifa hiyo imeeleza shughuli zote za mazishi zitakuwa katika Msikiti wa Maamur leo Jumamosi.
Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa maziko yatakuwa kesho Jumapili tarehe 5 Mei 2024 Kilosa mkoani Morogoro.
Mkulo ambaye alikuwa ni mbunge mstaafu, aliongoza kwa miaka 10 jimbo la Kilosa na katika kipindi hicho alishika nafasi ya waziri wa fedha kuanzia mwaka 2007 hadi 2012 alipotemwa na Rais Jakaya Kikwete.
Mkulo alitangaza kutogomea tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na nafasi yake ikachukuliwa na Mbunge Mbaraka Bawaziri.
Leave a comment