Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa
Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the love

ALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa Mkulo amefariki dunia leo tarehe 4 Mei 2024 katika hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti  Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na mke wa marehemu, Julie Mkulo msiba upo nyumbani kwa marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, taarifa hiyo imeeleza shughuli zote za mazishi zitakuwa katika Msikiti wa Maamur leo Jumamosi.

Taarifa hiyo pia imeeleza kuwa maziko yatakuwa kesho Jumapili tarehe 5 Mei 2024 Kilosa mkoani Morogoro.

Mkulo ambaye alikuwa ni mbunge mstaafu, aliongoza kwa miaka 10 jimbo la Kilosa na katika kipindi hicho alishika nafasi ya waziri wa fedha kuanzia mwaka 2007 hadi 2012 alipotemwa na Rais Jakaya Kikwete.

Mkulo alitangaza kutogomea tena katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na nafasi yake ikachukuliwa na Mbunge Mbaraka Bawaziri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Uingereza yamwaga bil. 9 kumuunga mkono Samia matumizi nishati

Spread the loveWaziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe abadili mbinu ya kudai Katiba mpya

Spread the loveMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Fremaan Mbowe amebadili mbinu...

error: Content is protected !!