Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Moshi mweupe duru ya 3 mazungumzo Urusi, Ukraine
Kimataifa

Moshi mweupe duru ya 3 mazungumzo Urusi, Ukraine

Spread the love

DURUya tatu ya mazungumzo kutoka kwa wajumbe wa nchi za Ukraine na Urusi, imepiga hatua na kusababisha Urusi kutangaza njia salama kwa raia wanaotaka kuondoka nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Hatua hiyo imekuja baada ya duru ya kwanza na ya pili ya mazungumzo hayo yanayofanyika nchini jirani ya Belarusi kugonga mwamba.

Duru hiyo ya tatu ya mazungumzo yanayolenga kusitisha vita kati ya nchi Ukraine na Urusi ilimalizika jana jioni ya tarehe 7 Machi, 2022.

Mmoja wa maofisa wa Serikali wa Ukraine, amenukuliwa na Shirika la habari la Interfax akisema kumepatikana maendeleo madogo ambayo hakuyataja.

Hata hivyo, baada ya mazungumzo hayo, Urusi ilitangaza kuruhusu raia kuondoka kwenye miji ya Ukraine, ukiwemo mji mkuu, Kyiv, kuanzia saa 3:00 asubuhi ya leo tarehe 8 Machi, 2022.

Aidha, raia hao walitakiwa kutumia njia zinazopitia Urusi na Belarusi kuondoka nchini Ukraine jambo ambalo Ukraine imelikataa.

Imeelezwa kuwa raia wanaoondoka miji ya Kyiv, Chernigov na Kharkiv walitakiwa kuelekea Urusi kupitia Belarus.

Hata hivyo, watu wanaoondoka kwenye mji wa Sumy na Mariupol wamepewa fursa ya kuchagua ama kupitia Urusi au miji ya Ukraine ya Potlava na Zaporizhia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!