Friday , 10 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Corona yaua 10,000 sikukuu za Krismasi, mwaka mpya
AfyaKimataifa

Corona yaua 10,000 sikukuu za Krismasi, mwaka mpya

Spread the love

Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO), Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema mikusanyiko ya sikukuu za mwisho wa mwaka imesababisha kasi ya kusambaa kwa virusi vya COVID-19 dunia vilivyosababisha vifo vya watu 10,000 Disemba mwaka jana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Ghebreyesus alisema karibu vifo 10,000 viliripotiwa mwezi Disemba, wakati watu waliolazwa hospitali katika mwezi huo waliongezeka kwa asilimia 42 katika nchi takribani 50, hasa za Ulaya na Marekani ambazo zilishirikiana taarifa kama hizo.

Ijapokuwa vifo 10,000 kwa mwezi ni kidogo sana kuliko wakati janga hili lilipoanza, kiwango hiki cha vifo vinavyoweza kuzuilika hakikubaliki,” alisema mkurugenzi huyo wa WHO alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Geneva nchini Uswis.

Alisema ni uhakika kwamba visa vinaongezeka katika maeneo mengine ambayo hayajaripoti.

Pia ametoa wito kwa serikali kuendelea kufuatilia na kutoa fursa ya kuendelea kupata matibabu na chanjo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!