Hatimaye Rais Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Dk. Edwin P. Mhede aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi yaendayo Haraka (DART). Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Dk. Mhede ambaye imeelezwa atapangiwa kazi nyingine, nafasi yake imechukuliwa na Dk. Athuman Kihamia aliyewahi kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha.
Hatua hiyo inajiri baada ya kuzorota kwa muda mrefu kwa huduma za usafiri wa mabasi hayo jijini Dar es Salaam na kuzidisha adha ya usafiri kwa wakazi wa jiji hilo huku uongozi wa Dart ukiendelea kukaa kimya bila kuchukua hatua zozote.
Aidha, taarifa iliyotolewa leo Alhamisi na Mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu, Zuhura Yunus pia Rais Samia amemteua Musa N. Kuji kuwa Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA). Kuji alikuwa akikaimu nafasi hiyo.
Leave a comment