Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa (WHO), Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema mikusanyiko ya sikukuu za mwisho wa mwaka imesababisha kasi ya kusambaa kwa virusi vya COVID-19 dunia vilivyosababisha vifo vya watu 10,000 Disemba mwaka jana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Ghebreyesus alisema karibu vifo 10,000 viliripotiwa mwezi Disemba, wakati watu waliolazwa hospitali katika mwezi huo waliongezeka kwa asilimia 42 katika nchi takribani 50, hasa za Ulaya na Marekani ambazo zilishirikiana taarifa kama hizo.
Ijapokuwa vifo 10,000 kwa mwezi ni kidogo sana kuliko wakati janga hili lilipoanza, kiwango hiki cha vifo vinavyoweza kuzuilika hakikubaliki,” alisema mkurugenzi huyo wa WHO alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Geneva nchini Uswis.
Alisema ni uhakika kwamba visa vinaongezeka katika maeneo mengine ambayo hayajaripoti.
Pia ametoa wito kwa serikali kuendelea kufuatilia na kutoa fursa ya kuendelea kupata matibabu na chanjo.
Leave a comment