Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kamati Kuu Chadema kuketi Mei 11
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kamati Kuu Chadema kuketi Mei 11

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa kuketi katika makao makuu ya chama hicho, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 11 Mei 2024. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 9 Mei 2024 na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje Chadema, John Mrema

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, masuala matatu yanatarajiwa kuteka kikao cha kamati hiyo, ikiwemo taarifa ya uchaguzi katika ngazi mbalimbali za chama hicho.

“Kamati Kuu itakuwa na mambo yafuatayo, kupokea taarifa ya chaguzi katika ngazi mbalimbali za chama, kupokea tathimini ya maandamano ya awamu ya kwanza ya mikoa  katika wiki ya maandamanona kuweka mwelekeo wa awamu ya pili ya maandamano,” imesema taarifa ya Mrema.

Suala lingine litakalofanyiwa kazi kwenye kikao hicho ni kufanya usaili na kuteua wagombea nafasi mbalimbali katika chaguzi za kuwatafuta viongozi wa kanda nne za Chadema,  Nyasa, Serengeti, Victoria na Magharibi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Elimu ya utunzaji wa mazingira ipewe kipaumbele kwa watoto

Spread the love  JAMII imetakiwa kuwajengea Watoto tabia ya utunzaji wa mazingira...

Habari za SiasaKimataifa

Kiongozi Mkuu Iran amteua mrithi wa Rais Ebrahim

Spread the loveKiongozi wa ngazi ya juu nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei,...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 85,471 walioenguliwa kipindi cha JPM wapandishwa vyeo

Spread the loveSERIKALI imesema kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

error: Content is protected !!