KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa kuketi katika makao makuu ya chama hicho, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, kuanzia tarehe 11 Mei 2024. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 9 Mei 2024 na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje Chadema, John Mrema
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, masuala matatu yanatarajiwa kuteka kikao cha kamati hiyo, ikiwemo taarifa ya uchaguzi katika ngazi mbalimbali za chama hicho.
“Kamati Kuu itakuwa na mambo yafuatayo, kupokea taarifa ya chaguzi katika ngazi mbalimbali za chama, kupokea tathimini ya maandamano ya awamu ya kwanza ya mikoa katika wiki ya maandamanona kuweka mwelekeo wa awamu ya pili ya maandamano,” imesema taarifa ya Mrema.
Suala lingine litakalofanyiwa kazi kwenye kikao hicho ni kufanya usaili na kuteua wagombea nafasi mbalimbali katika chaguzi za kuwatafuta viongozi wa kanda nne za Chadema, Nyasa, Serengeti, Victoria na Magharibi.
Leave a comment