Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%
Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the love

SERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia 30 hadi 10, kwa kipindi cha miaka mitano ya mwanzo, lengo likiwa ni kuchochea uwekezaji katika sekta ya viwanda. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamesemwa leo tarehe 9 Mei 2024 na Rais Samia Suluhu Hassan, akizindua kiwanda cha kuunganisha malori na matipa cha Saturn Corporation Limited, Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Mkuu huyo wa nchi amesema Serikali yake itaendelea kujenga uchumi wa kisasa, fungamanishi, jumuishi na shindanishi katika msingi wa viwanda, huduma za kiuchumi na miundombinu wezeshi.

Rais Samia amesema sekta hiyo inaongeza uzalishaji na kutoa ajira kwa wananchi na kukuza uchumi jumuishi na kusaidia kuondoa umasikini.

Kuhusu kiwanda hicho cha kuunganisha malori, Rais Samia amesema bidhaa zitakazozalishwa zinasaidia kupunguza gharama pamoja na kutoa ajira za moja kwa moja 250 na zisizo za moja kwa moja 1,800.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Elimu ya utunzaji wa mazingira ipewe kipaumbele kwa watoto

Spread the love  JAMII imetakiwa kuwajengea Watoto tabia ya utunzaji wa mazingira...

Habari za SiasaKimataifa

Kiongozi Mkuu Iran amteua mrithi wa Rais Ebrahim

Spread the loveKiongozi wa ngazi ya juu nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei,...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 85,471 walioenguliwa kipindi cha JPM wapandishwa vyeo

Spread the loveSERIKALI imesema kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

error: Content is protected !!