Friday , 10 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri aburuzwa kortini kwa kuuza mabati ya msaada
Kimataifa

Waziri aburuzwa kortini kwa kuuza mabati ya msaada

Spread the love

 

MAHAKAMA nchini Uganda imemfungulia rasmi mashtaka ya ufisadi na rushwa Waziri Marie Goretti Kitutu kutokana na tuhuma za kuuza mabati 14,500 ya kuezekea nyumba yaliyokusudiwa kuwasaidia raia wa huko Karamoja. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Licha ya Waziri Kitutu kukana mashtaka hayo, alirejeshwa rumande na kesi yake itasikilizwa tena ifikapo tarehe 12 Aprili mwaka huu.

Akihojiwa na Kamati ya Bunge mwezi uliopita, Marie Goretti Gitutu aliomba msamaha kwa usimamizi mbaya wa usambazaji wa mabati hayo.

Mawaziri kushtakiwa kwa ufisadi ni jambo la nadra nchini Uganda, ambako ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma ni jambo lililozoeleka.

Karamoja ni eneo la Uganda linalopakana na mataifa ya Kenya na Sudan Kusini, na wakazi wake ni wafugaji wanaohamahama ambao wako katika hatari ya kukumbwa na ukame na wizi wa mifugo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!