Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri aburuzwa kortini kwa kuuza mabati ya msaada
Kimataifa

Waziri aburuzwa kortini kwa kuuza mabati ya msaada

Spread the love

 

MAHAKAMA nchini Uganda imemfungulia rasmi mashtaka ya ufisadi na rushwa Waziri Marie Goretti Kitutu kutokana na tuhuma za kuuza mabati 14,500 ya kuezekea nyumba yaliyokusudiwa kuwasaidia raia wa huko Karamoja. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Licha ya Waziri Kitutu kukana mashtaka hayo, alirejeshwa rumande na kesi yake itasikilizwa tena ifikapo tarehe 12 Aprili mwaka huu.

Akihojiwa na Kamati ya Bunge mwezi uliopita, Marie Goretti Gitutu aliomba msamaha kwa usimamizi mbaya wa usambazaji wa mabati hayo.

Mawaziri kushtakiwa kwa ufisadi ni jambo la nadra nchini Uganda, ambako ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma ni jambo lililozoeleka.

Karamoja ni eneo la Uganda linalopakana na mataifa ya Kenya na Sudan Kusini, na wakazi wake ni wafugaji wanaohamahama ambao wako katika hatari ya kukumbwa na ukame na wizi wa mifugo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!