Friday , 10 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema
Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Wakili Boniface Mwabukusi
Spread the love

 

KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi, Sauti ya Watanzania, kimesema kimechagua kukiunga mkono Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa kuwa kina nia ya dhati kutatua matatizo ya wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Sababu hiyo imetajwa leo tarehe 27 Aprili 2024, na mwanachama wa kikundi hicho, Boniface Mwabukusi, akizungumza katika mkutano wa hadhara wa Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu, uliofanyika mkoani Singida.

“Tunaiunga mkono Chadema kwa sababu ya namna inavyojiweka, hata watoto wanalia njaa unaangalia nani anayelia sana ndiyo mwenye njaa. Tunaiunga mkono Chadema kwa sababu kazi kubwa wanayofanya. Chadema ndiyo chama pekee utakuta kina wanachama ambao wanatumia gharama zao kujenga demokrasia,” amesema Mwabukusi.

Akizungumzia maandamano yanayofanywa na Chadema maeneo mbalimbali, Mwabukusi amesema yanafanyika kwa wakati sahihi kwa kuwa yanalengo la kudai katiba mpya itakayoleta mgawanyo wa madaraka kati ya Bunge, mahakama na Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!