Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Lori laparamia na kuua madereva bodaboda 10
Kimataifa

Lori laparamia na kuua madereva bodaboda 10

Spread the love

WATU 10 wanadaiwa kupoteza maisha baada ya lori lililokuwa likisafirisha changarawe kupoteza mwelekeo na kuparamia kijiwe cha bodaboda katika eneo lao mjini Migori nchini Kenya. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Waliopoteza maisha katika ajali hiyo iliyotokea leo tarehe 8 Aprili 2023, inaelezwa ni vijana wa bodaboda waliokuwa wakisubiria wateja kwenye kijiwe chao.

Umati mkubwa wa watu ulimiminika eneo la tukio ili kuwanusuru majeruhi na kuwakimbiza hospitalini kwa matibabu.

Kwa mujibu wa raia mmoja aliyeshuhudia na kuzungumza na runinga ya TV47, breki za lori hilo zilifeli na kuingia katika kundi hilo la bodaboda ambao walikuwa wanasubiri abiria.

Ajali hiyo imetokea karibu na shule ya msingi ya Migori. Eneo la tukio lilikuwa limejaa damu na miili. Vyuma pia vilikuwa vimetapakaa eneo hilo.

Eneo la tukio linaripotiwa kuwa na zaidi ya miili 10 huku gari za kubeba wagonjwa ‘ambulansi’ na zima moto kutoka kwa serikali ya kaunti ya Migori zikifika eneo la ajali hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!