Sunday , 12 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Maofisa 10 TEA watokomea na mkopo wa mamilioni
Habari Mchanganyiko

Maofisa 10 TEA watokomea na mkopo wa mamilioni

Spread the love

RIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere imeonyesha mikopo yenye thamani ya Sh milioni 167 haijarejeshwa na wafanyakazi katika Mamlaka ya Elimu Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Ripoti hiyo ya mwaka wa fedha 2021/2022  iliyowasilishwa bungeni juzi tarehe 6 Aprili  2023 jijini Dodoma, ilisema maofisa 10 wanadaiwa shilingi milioni 167 kwa kipindi cha kuanzia mwaka mmoja hadi 10 bila ya mpango madhubuti wa kurejesha mikopo hiyo.

Imesema mikopo hiyo imebaki bila kulipwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo uhamisho na kustaafu kwa maofisa.

Hata hivyo, imesema uongozi ulieleza kuwa hatua zaidi zimepangwa kuchukuliwa ili kurejesha mkopo uliobaki ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua za kisheria.

“Kwa maoni yangu, ikiwa mikopo haitarudishwa kwa wakati, Mamlaka itapata hasara. Ninapendekeza Mamlaka ya Elimu Tanzania ichukue hatua stahiki katika kukusanya mikopo iliyosalia ya wafanyakazi,” imesema ripoti hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

BiasharaHabari Mchanganyiko

PPAA yajipanga kuwanoa wazabuni namna kuwasilisha rufaa kieletroniki

Spread the loveIli kukabiliana na mageuzi yaliyofanyika katika Sheria mpya ya Ununuzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!