Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Urusi, Ukraine zabadilishana wafungwa wa kivita
Kimataifa

Urusi, Ukraine zabadilishana wafungwa wa kivita

Spread the love

JUMLA ya wafungwa 179 wa kivita wa Urusi na Ukraine wamerejea nyumbani kufuatia mpango wa kubadilishana wafungwa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Mshauri mwandamizi katika ofisi ya Rais Ukraine,  Andriy Yermak amesema wanajeshi 116 wa nchi hiyo wameachiliwa huru.

Amesema wafungwa wa kivita walioachiwa wanajumuisha waliokuwa katika mji wa Mariupol wakati wa mzingiro wa miezi kadhaa wa Moscow, pamoja na wapiganaji kutoka mkoa wa Kherson na walenga shabaha waliokamatwa wakati wa mapambano makali yanayoendelea ya kuudhibiti mji wa mashariki wa Bakhmut.

Kwa upande mwingine, Maofisa wa ulinzi wa Urusi nao wametangaza kuwa askari 63 wa Urusi wamerejea nyumbani kutoka Ukraine kufuatia ubadilishanaji huo wa wafungwa.

Kati ya wafungwa hao wamo waliotajwa kuwa kutoka kitengo maalum ambao kuwachiwa kwao kulitokana na mazungumzo ya upatanishi na Umoja wa Falme za Kiarabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!