WAKATI Chama Cha Mapinduzi leo tarehe 5 Februari 2023 kikitimiza miaka 46 tangu kuasisiwa kwake, Rais Samia Suluhu Hassan ametumia ukurasa wake wa Twitter kutoka pongeza kwa wanachama na chama hicho na Watanzania kwa kutimiza miaka hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Rais Samia ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho ameandika; “Pongezi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kutimiza miaka 46. Pongezi kwa wana CCM na Watanzania wote. Busara na maono ya waasisi wetu viliunganisha TANU na ASP kutujengea chama hiki chenye misingi imara, kinachoendelea na kazi adhimu ya kuwatumikia Watanzania, Awamu hadi Awamu”.
CCM kiliasisiwa mwak 1977 baada ya vyama hivyo vya TANU na ASP kuungana chini ya uongozi wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Leave a comment