JUMLA ya wafungwa 179 wa kivita wa Urusi na Ukraine wamerejea nyumbani kufuatia mpango wa kubadilishana wafungwa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Mshauri mwandamizi katika ofisi ya Rais Ukraine, Andriy Yermak amesema wanajeshi 116 wa nchi hiyo wameachiliwa huru.
Amesema wafungwa wa kivita walioachiwa wanajumuisha waliokuwa katika mji wa Mariupol wakati wa mzingiro wa miezi kadhaa wa Moscow, pamoja na wapiganaji kutoka mkoa wa Kherson na walenga shabaha waliokamatwa wakati wa mapambano makali yanayoendelea ya kuudhibiti mji wa mashariki wa Bakhmut.
Kwa upande mwingine, Maofisa wa ulinzi wa Urusi nao wametangaza kuwa askari 63 wa Urusi wamerejea nyumbani kutoka Ukraine kufuatia ubadilishanaji huo wa wafungwa.
Kati ya wafungwa hao wamo waliotajwa kuwa kutoka kitengo maalum ambao kuwachiwa kwao kulitokana na mazungumzo ya upatanishi na Umoja wa Falme za Kiarabu.
Leave a comment