Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri mkuu Uingereza agoma kujiuzulu
Kimataifa

Waziri mkuu Uingereza agoma kujiuzulu

Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson ameendelea kusisitiza kuwa hatojiuzulu licha ya kuendelea kushinikizwa kufanya hivyo kutokana na kashfa mbalimbali zinazoiandama serikal yake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kashfa hizo zimesababisha baadhi ya maofisa wa serikali, Waziri wa afya, Sajid Javid na waziri fedha Rishi Sunak kujiuzulu kwa kile wanachosema hawana imani na Waziri Mkuu Boris.

Hayo yanajiri baada ya Waziri mkuu huyo kuomba radhi kwa kile alichokieleza kuwa hakufahamu kuwa mmoja wa wafanyakazi wa serikali, ambaye pia ni Waziri wa zamani, alihusika na utovu wa nidhamu wa kingono, pia nay eye binafsi kufanya sherehe na kukiuka masharti ya corona kipindi hicho.

Jana tarehe 7 Julai, 2022 Johnson amewambia wabunge kwamba ataendelea kutekeleza majukumu yake, licha ya shinikizo hilo.

Aidha, mawazi kadhaa wakiwemo wandani wake Johnson, kama vile waziri wa uchukuzi Grant Shapps, wanatarajiwa kuandaa kikao naye kumshawishi ajiuzulu.

Katika hatua nyingine Johnson amemfuta kazi mmoja wa mawaziri wake Michael Gove, huku chama chake cha Conservative kikitarajiwa kukutana wiki ijayo kuangalia upya kanuni za chama ili kuitisha kura ya kukosa imani naye, wakati ou huo waziri mweingine Simon Hart, pia amejiuzulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!