Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine kuhudhuria kikao cha Baraza kuu la Chadema
Kimataifa

Bobi Wine kuhudhuria kikao cha Baraza kuu la Chadema

Robert Kyagulanyi 'Bobi Wine'
Spread the love

 

KIONGOZI wa Upinzani nchini Uganda Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine,anatarajia kuwa mgeni maalum katika kiakao cha Baraza Kuu la Chadema litakalofanyika jumatano tarehe 11 mei 2022. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea),

Ujio huo umethibitishwa na Mkurugenzi wa Itifaki,Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema leo jumatatu tarehe 9 mei 2022,wakati akizungumza na waandishi kuhusu maandalizi ya kikao hicho, kitakachotanguliwa na kikao cha kamati kuu itakayoketi kesho jumanne mei 10 2022.

Chadema kitafanya kikao cha baraza kuu tarehe 11 Mei 2022, kitakacho kuwa na ajenda tano na kuhudhuriwa na wajumbe zaidi ya 400 wa chama hicho, watakaotoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania bara na Zanzibar.

Aidha Bobi Wine aligombea urais wa Uganda, kwa tiketi ya chama cha National Unity (NUP), platform katika uchaguzi uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!