Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani kutoa dola 100 kwa atakayekubali chanjo ya Korona
Kimataifa

Marekani kutoa dola 100 kwa atakayekubali chanjo ya Korona

Joe Biden, Rais wa Marekani
Spread the love

 

RAIS wa Marekani, Joe Biden ameanzisha utaratibu wa kutoa dola 100 (Sh.231900), kwa kila mwananchi atakaye kubali kuchanjwa chanjo ya Ugonjwa wa Korona, ikiwa ni jitihada za kutokomeza maambukizi ya wimbi la tatu la janga hilo, nchini humo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Biden ametangaza uamuzi huo jana tarehe 29 Julai 2021, akilihutubia Taifa hilo akiwa Ikulu ya White House, Marekani.

Rais huyo wa Marekani, aliagiza maafisa wa Serikali za mitaa nchini humo, kutoa fedha hizo kama motisha kwa watu watakaokubali chanjo hiyo.

Rais Biden alisema kuwa, uamuzi huo utawafanya wananchi wa Marekani, kuwa na mwamko wa kupata chanjo kuliko kutumia nguvu.

Pia, Rais Biden aliagiza watumishi wa Marekani, kutoa vielelezo vinavyoonesha kama wamepata chanjo ya Korona.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!